Search This Blog

Friday, 1 April 2016

ELIMU YA UJASILIAMALI JUU YA UKULIMA WA MAHINDI

Upandaji  wa  Mahindi
1.  Mbegu   Upandaji  wa mahindi  unatakiwa ufanyike pale tu mvua  zinapoanza kunyesha,  kuchelewa kupanda  mahindi  kwa siku  moja hupunguza  uzalishaji  wa  mmea  kwa  asilimia  1  hadi  2.  Kupanda  mbegu  za  mahindi  katika  hecta  moja  kwa  mkono kunahitaji  angalau  siku tano hadi  kumi. Mbegu huwekwa kwenye shimo lenye urefu wa sentimita tano ili  kuzuia kuchipua kutokana na mvua zisizo za kweli. Kwa ekari moja kilo 8 hadi 10 za mbegu za mahindi zitahitajika na kilo 25 kwa hecta. Ili  kuwa  na  mahindi  yaliyosimama  vizuri,  inashauriwa  kuacha  nafasi  ya  sentimita  75  (mstari  kwa  mstari)  na  sentimita  30 (mbegu  kwa  mbegu)  ambazo  zitatoa  mazao  ya  mahindi  44,000  kwa  hecta  moja  katika  maeneo  yenye  mvua  za  kutosha. Au  unaweza  kuweka  nafasi  ya  75×25  ambayo  itatoa  mimea  53,000  kwa  hecta  moja.  Katika  maeneo  ambayo  ni  makavu sana inashauriwa kuongeza ukubwa wa nafasi hadi angalau 90×30.
2.  Magugu Kupalilia  mahindi  kunatakiwa  kufanyike  wiki  4  hadi  6  za  mwazo  baada  ya  kujitokeza  kwani  magugu  husababisha uharibifu mkubwa katika mahindi kwa kuchukua virutubisho ambavyo vingetumika kama chakula cha mmea. i)  Gugu  chawi/sani  (striga)                                      ii)Bungua  weupe  wa  kahawia  (stalk borer)            
    3.  Mbolea
iii) Bungua/viwavi/Funza (stem borer) Mbolea  ambazo zina chumvi  chumvi  na  zenye kuyeyuka haraka kwenye  maji  huleta madhara yafuatayo:   Huzuia viumbehai  kukua  hivyo kuharibu udongo.   Hulazimisha  mimea  kutumia hizi  chumvi  chumvi  hata  kama  mimea  haizihitaji.   Mimea inapotumia  hizi  chumvi  chumvi  kwa  kulazimishwa  ukuaji  wake  huvurugika  na  kusababisha  upungufu  wa afya na  kinga hivyo kufanya  mimea  iweze kuathiriwa  na magonjwa pamoja na  wadudu. Inashauriwa  kutumia  mbolea  ambazo  ni  endelevu/hai  na  haziyeyuki  haraka  kwenye  maji  kwa  mfano  samadi,  mboji  na mabaki  ya  mimea  ambazo  ni  nzuri  kwa  udongo,  mimea,  mazingira,  afya  na  faida  zake  ni  za  muda  mrefu.  Kama  ukitumia samadi  au  mboji,  inashauriwa  kuchanganya  mbolea  hizi  katika  udongo  kabla  ya  kupanda  mahindi  ili  kusaidia  kurutubisha ardhi  na  kuupa  mmea  chakula  na  nguvu,  baada  ya  mimea  kuota  inatakiwa  kuendelea  kuweka  mbolea  hizi  mara  kwa  mara. Pia  mbolea  hai/endelevu  husaidia  kuhifadhi  unyevu  nyevu  na  kupunguza  ukaukaji  wa  udongo.  Madini  ya  nitrogen, phosphorous  na  potassium  hupatikana  kwenye  mbolea  hai  kama  vile  samadi,  mboji,  mimea  mibichi  yenye  uwezo  wa kutengeneza  nitrogen,  mkojo  wa  mnyama  na  majivu.  Inashauriwa  kuhakikisha  kuwa  udongo  wako  unapitisha  hewa  ya kutosha ili kusaidia viumbehai waishio kwenye udongo wanaozalisha hivi virutubisho kuweza kukua.
4.  Kukomaa na kuvuna Kukomaa  kwa  mahindi  hutofautiana  kutokana  na  aina  ya  mbegu  iliyotumika.  Lakini  mahindi  mengi  huwa  yamekomaa baada  ya  miezi  mitano  hadi  saba.  Majani  ya  muhindi  yakianza  kukauka  ni  ishara  kuwa  mahindi  yamekomaa  na inashauriwa  kuyavuna  mara  moja  na  kuyahifadhi  vizuri  ili  kuzuia  hasara  ambazo  zitatokea  kutokana  na  kuharibiwa  na magonjwa au wadudu shambani kama yakicheleweshwa.

Kilimo  Mseto (mchanganyiko) Kilimo  mseto  (mchanganyiko)  ni  aina  ya  kilimo  ambayo  inajumuisha  kupanda  mazao  mawili  au  zaidi  kwenye  shamba moja  katika  wakati  mmoja.  Aina  hii  ya  kilimo  inajumuishwa  na  kilimo  hai  au  kilimo  endelevu  na  inafanyika  katika maeneo  mengi.  Katika  kilimo  mchanganyiko,  zao  moja  huwa  muhimu  kwasababu  za  kiuchumi  au  chakula  na  zao  jingine au mazao mengine hupandwa ili kusaidia hilo zao muhimu.  Dhumuni  la  kupanda  mmea  zaidi  ya  mmoja  kwenye  shamba  ni  kuongeza  mavuno  kutoka  shambani  kwa  kutumia  ardhi ambayo  isingeweza  kutumika  yote  kupanda  mmea  mmoja.  Ni  muhimu  kufanya  tathmini  ya  kina  ili  kuhakikisha  kuwa mimea haitagombania maji, mwanga wa jua, nafasi ya kukulia na virutubisho vingine kutoka katika udongo. Namna  moja wapo ya kilimo  mseto/mchanganyiko  ni  kupanda  mmea  wenye  mizizi  mirefu pamoja na mmea  wenye  mizizi mifupi  au  kupanda  mmea  mrefu  wenye  kuhitaji  jua  pamoja  na  mmea  mfupi  ambao  hauhitaji  sana  jua.  Hapa  mmea  mrefu utausaidia mmea  mfupi  kwa kuukinga na  mwanga wa moja kwa moja kutoka kwenye jua.   Miongoni  mwa  mazao  ambayo  yanaweza  kupandwa  pamoja  na  mahindi  ni  pamoja  na  Maharage,  Njegere,  karanga  na Soya (jamii ya kunde). Namna ya  kilimo mseto  kwaajili  ya kufukuza  wadudu  na kuzuia magugu  (Sukuma-Vuta) Sukuma-Vuta  ni  mfumo  wa  kilimo  ambao  hutumika  katika  kufukuza  wadudu  waharibifu  na  kuzuia  magugu  maharibifu kwenye  mahindi.  Mfumo  huu  ni  rahisi  na  nafuu  kuunda.  Itahitaji  kuwa  na  majani  ya  Napier/Elephant  grass  (matembo tembo) na Desmodium katika kutengeneza huu mfumo. Desmodium  hupandwa  katikati  ya  mistari  ya  mahindi  na  hutoa  harufu  ambayo bungua/viwavi  (stem  borer)  hawaipendi  hivyo  kuwafanya  wasije  kwenye  mahindi. Napier  grass  (matembo  tembo)  hupandwa  kuzunguka  matuta  ya  mahindi,  hutumika  kama mtego  wa  bungua/viwavi  (stem  borer)  kwani  bungua  hupendelea  zaidi  haya  majani kuliko  mahindi  na  huvutwa  kutaga  mayai.  Lakini  matembo  tembo  hayaruhusu  bungua wadogo  waliototolewa  kukua  hivyo  hutoa  kitu  fulani  kama  gundi  ambayo  huwanasa.  Hii husababisha  kutokukua  kwa  bungua  na  hivyo  kupunguza  uharibifu  na  hasara  katika mahindi. Desmodium  pia  hutumika  kuzuia  magugu  kama  vile  striga  (gugu  chawi/sani)  ambayo  ni  maharibifu  kuota.  Tafiti zinaonyesha  kuwa  majimaji  ambayo  hutolewa  na  desmodium  huzuia  striga  na  hivyo  striga  haziwezi  kuota  sehemu ambayo  desmodium  inaota.  Pia  desmodium  husaidia  kuongeza  madini  ya  nitrogen  kwenye  udongo  ambayo  ni  muhimu kwa mahindi kukua na kuzaa. Namna ya kutengeneza mfumo  wa Sukuma-Vuta
 1.  Panda majani  ya Napier  (matembo tembo)  kwenye  mipaka ya shamba lako la mahindi.
2.  Weka angalau mistari  mitatu ya  matembo tembo na angalau mikono  miwili  ya samadi  kwenye kila shimo.
 3.  Katika mwaka wa  kwanza,  panda  matembo tembo kabla ya mvua ili  yaanze kuota  kabla ya mahindi.
4.  Pata  mbegu  au  vijiti  vya  desmodium  na  kuvipanda,  kama  utatumia  mbegu  kwa  ekari  moja  kilo  moja  ya  mbegu itahitajika na  kama utatumia vitawi  basi  hakikisha  kuwa kuna mvua ya  kutosha  na  udongo una unyevunyevu.
5.  Tayarisha udongo kwa makini  ili  kuhakikisha  kuwa uko  vizuri  kisha  changanya  mbegu za desmodium.
 6.  Tumia fimbo/kijiti  kigumu  kilichochongeka kuweka  mitaro katika matuta ambapo  mahindi  yatapandwa.
7.  Panda mbegu za  mahindi  kwenye shamba lililozungukwa na  matembo tembo.
 8.  Baada ya wiki  3 hadi  6,  katia majani  ya desmodium  ili  yasizidi  katika mahindi. 9.  Hakikisha  shamba  halina  magugu  mengine  ili  matembo  tembo  yaanze  pamoja  na  mahindi.  Bungua  watapendelea zaidi matembo tembo kuliko mahindi. Faida za kutumia  mfumo  wa Sukuma-Vuta   Kuongeza  mavuno  ya  mahindi  kwa  asilimia  25  hadi  30  katika  maeneo  ambayo  bungua/viwavi  (stem  borer)  ni tatizo sugu. Kama  tatizo ni  bungua na  striga unaweza kuongeza  mavuno  mara mbili  zaidi.     Kuongeza lishe  ya ng’ombe kwa  kutumia  majani  ya matembo tembo na desmodium.   Kuongeza madini  ya nitrogen kwenye udongo ambayo  ni  muhimu kwa  mahindi.   Kubakisha unyevu nyevu na kuongeza rutuba  kwenye udongo kwa kutumia majani  ya desmodium.   Kupungua kwa kazi  ya kupalilia kwani  magugu hupungua au kutoota kabisa.  Kukinga mahindi kwa kutumia matembo tembo kuzuia upepo mkali.

No comments:

Post a Comment